Thursday, June 12, 2008
Monday, May 19, 2008
CAST PLANT
Huu ni mmea ambao umezoeleka kuonekana maeneo mengi ya Tanzania, mme huu hutoa mbegu ambazo zinatoa mafuta (cast oil) kiasi cha 40% - 60%. Mafuta haya yanakuwa na kemikali ya recin ambayo ni sumu.
Sumu iliyomo kwenye mbegu za mimea hii inauwezo wa kuua binadamu kwa kiasi kidogo chambegu 2 - 3 kwa mtoto mdogo ma mbegu 8 kwa mtu mzima
MATUMIZI
Mafuta haya yanauwezo mkubwa wa kutibu fangasi za miguu, maonjwa ya ngozi na miguu kupasuka, pia yanasaidia kufunga choo kwa wale wenye tatizo hili lakini yanywewe katika kiwango kidogo sana kwa sababu ni sumu
Saturday, May 03, 2008
KOBE-TORTOISE
Huyu ni kiumbe rahisi sana kumfuga kwa sababu joto la mwili wake linarekebishika kutegemeana na mazingira (ectothemic)
MAZINGIRA
Unaweza kumfuga ndani ya nyumba, lakini ni vizuri sana kama utamweka mazingira nje. Mazingira yawe makavu na upande mwingine kuwe na bwawa dogo la maji, haya maji ni ya kunywa na wale kobemaji hupenda kuogelea humo. Hakikisha wapo katika mazingira masafi kwa sababu wanauwezo wa kubeba vijidudu vya magonjwa yanayodhuru binadamu.
CHAKULA
Ukimfuga katika mazingira asili ya nje ataweza kujitafutia chakula chake na wewe utamwongezea kidogo tu cha ziada (concentrates)
Kobe kwa kawaida hula majani na mboga mboga, uyoga, wadudu na minyoo. Pia unaweza kuwapa chakula cha mbwa (kidogo) kama chakula cha ziada.
Friday, April 25, 2008
Saturday, January 05, 2008
MKARATUSI NA UKWAJU (eucalyptus & tamarind) TIBA YA KIFUA
Mikaratusi na ukwaju ni tiba yenye nguvu dhidi ya kifua na kukohoa, tiba hii ni rahisi kuandaa na haina gharama.
UAANDAAJI
Chukua jani moja au zaidi ya mkaratusi lililokomaa kotoka katika matawi machanga/mapya ya mti, ponda ponda na uchuje kwenye maji kiasi cha mililita 100-200, unaweza kutumia blender pia kusagia dawa hii, kisha changanya na juisi ya ukwaju, pia unaweza kuongezea tangawizi kidogo ukipenda.
MATUMIZI
Kunywa mchanganyiko huu mara 3 kwa siku kwa siku 3-5
Ukitumia mchanganyiko huu mara moja kwa wiki ni kinga tosha kwa magonjwa ya njia ya hewa
NB Ukichemsha majani ya mkaratusi chumbani na kacha mvuke usambae chumbani ni kinga tosha juu ya mafua, pia huleta harufu nzuri chumbani (air freshener)
Friday, January 04, 2008
MBAAZI KAMA DAWA-cajanus cajan
Mbaazi ni zao la chakula ambalo linalimwa sehemu nyingi sana hapa nchini, zao hili pia linaweza kutumika kama dawa kwa kutumia majani, mizizi na maua
MAANDALIZI
Chukua majani, maua au mizizi kiasi cha nusu kilo (ni vizuri kama utachanganya vyote) pondaponda na uloweke kwenye maji safi kiasi cha lita 2 kwa muda wa masaa 24.
Chuja na uweke dawa hii mbali na jua/joto, ni vizuri kama ataweka kwenye friji, kunywa kikombe kimoja kutwa mara 3 kwa siku 3
TIBA
Dawa hii inaweza kutibu magonjwa yafuatayo
1-Inauwezo mkubwa wa kushusha homa
2-Husaidia kuponesha vidonda.
3-Husaidia kurekebisha mzunguko wa hedhi kwa wanawake.
4-Husaidia kupunguza uvimbe
5-Huponyesha kifua na kukohoa.
6-Husafisha kibofu/njia ya mkojo.
7- Huongeza kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbali mbali
Subscribe to:
Posts (Atom)