Thursday, June 12, 2008

Monday, May 19, 2008

CAST PLANT

Huu ni mmea ambao umezoeleka kuonekana maeneo mengi ya Tanzania, mme huu hutoa mbegu ambazo zinatoa mafuta (cast oil) kiasi cha 40% - 60%. Mafuta haya yanakuwa na kemikali ya recin ambayo ni sumu.


Sumu iliyomo kwenye mbegu za mimea hii inauwezo wa kuua binadamu kwa kiasi kidogo chambegu 2 - 3 kwa mtoto mdogo ma mbegu 8 kwa mtu mzima
MATUMIZI
Mafuta haya yanauwezo mkubwa wa kutibu fangasi za miguu, maonjwa ya ngozi na miguu kupasuka, pia yanasaidia kufunga choo kwa wale wenye tatizo hili lakini yanywewe katika kiwango kidogo sana kwa sababu ni sumu

Saturday, May 03, 2008

KOBE-TORTOISE


Huyu ni kiumbe rahisi sana kumfuga kwa sababu joto la mwili wake linarekebishika kutegemeana na mazingira (ectothemic)

MAZINGIRA
Unaweza kumfuga ndani ya nyumba, lakini ni vizuri sana kama utamweka mazingira nje. Mazingira yawe makavu na upande mwingine kuwe na bwawa dogo la maji, haya maji ni ya kunywa na wale kobemaji hupenda kuogelea humo. Hakikisha wapo katika mazingira masafi kwa sababu wanauwezo wa kubeba vijidudu vya magonjwa yanayodhuru binadamu.

CHAKULA
Ukimfuga katika mazingira asili ya nje ataweza kujitafutia chakula chake na wewe utamwongezea kidogo tu cha ziada
(concentrates)
Kobe kwa kawaida hula majani na mboga mboga, uyoga, wadudu na minyoo. Pia unaweza kuwapa chakula cha mbwa (kidogo) kama chakula cha ziada.

KUKU-(gallus gallus)


Friday, April 25, 2008

Saturday, January 05, 2008

MKARATUSI NA UKWAJU (eucalyptus & tamarind) TIBA YA KIFUA




Mikaratusi na ukwaju ni tiba yenye nguvu dhidi ya kifua na kukohoa, tiba hii ni rahisi kuandaa na haina gharama.
UAANDAAJI
Chukua jani moja au zaidi ya mkaratusi lililokomaa kotoka katika matawi machanga/mapya ya mti, ponda ponda na uchuje kwenye maji kiasi cha mililita 100-200, unaweza kutumia blender pia kusagia dawa hii, kisha changanya na juisi ya ukwaju, pia unaweza kuongezea tangawizi kidogo ukipenda.
MATUMIZI
Kunywa mchanganyiko huu mara 3 kwa siku kwa siku 3-5
Ukitumia mchanganyiko huu mara moja kwa wiki ni kinga tosha kwa magonjwa ya njia ya hewa
NB Ukichemsha majani ya mkaratusi chumbani na kacha mvuke usambae chumbani ni kinga tosha juu ya mafua, pia huleta harufu nzuri chumbani (air freshener)

Friday, January 04, 2008

MBAAZI KAMA DAWA-cajanus cajan









Mbaazi ni zao la chakula ambalo linalimwa sehemu nyingi sana hapa nchini, zao hili pia linaweza kutumika kama dawa kwa kutumia majani, mizizi na maua


MAANDALIZI

Chukua majani, maua au mizizi kiasi cha nusu kilo (ni vizuri kama utachanganya vyote) pondaponda na uloweke kwenye maji safi kiasi cha lita 2 kwa muda wa masaa 24.


Chuja na uweke dawa hii mbali na jua/joto, ni vizuri kama ataweka kwenye friji, kunywa kikombe kimoja kutwa mara 3 kwa siku 3


TIBA

Dawa hii inaweza kutibu magonjwa yafuatayo

1-Inauwezo mkubwa wa kushusha homa

2-Husaidia kuponesha vidonda.

3-Husaidia kurekebisha mzunguko wa hedhi kwa wanawake.

4-Husaidia kupunguza uvimbe

5-Huponyesha kifua na kukohoa.

6-Husafisha kibofu/njia ya mkojo.

7- Huongeza kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbali mbali