Monday, May 19, 2008

CAST PLANT

Huu ni mmea ambao umezoeleka kuonekana maeneo mengi ya Tanzania, mme huu hutoa mbegu ambazo zinatoa mafuta (cast oil) kiasi cha 40% - 60%. Mafuta haya yanakuwa na kemikali ya recin ambayo ni sumu.


Sumu iliyomo kwenye mbegu za mimea hii inauwezo wa kuua binadamu kwa kiasi kidogo chambegu 2 - 3 kwa mtoto mdogo ma mbegu 8 kwa mtu mzima
MATUMIZI
Mafuta haya yanauwezo mkubwa wa kutibu fangasi za miguu, maonjwa ya ngozi na miguu kupasuka, pia yanasaidia kufunga choo kwa wale wenye tatizo hili lakini yanywewe katika kiwango kidogo sana kwa sababu ni sumu

Saturday, May 03, 2008

KOBE-TORTOISE


Huyu ni kiumbe rahisi sana kumfuga kwa sababu joto la mwili wake linarekebishika kutegemeana na mazingira (ectothemic)

MAZINGIRA
Unaweza kumfuga ndani ya nyumba, lakini ni vizuri sana kama utamweka mazingira nje. Mazingira yawe makavu na upande mwingine kuwe na bwawa dogo la maji, haya maji ni ya kunywa na wale kobemaji hupenda kuogelea humo. Hakikisha wapo katika mazingira masafi kwa sababu wanauwezo wa kubeba vijidudu vya magonjwa yanayodhuru binadamu.

CHAKULA
Ukimfuga katika mazingira asili ya nje ataweza kujitafutia chakula chake na wewe utamwongezea kidogo tu cha ziada
(concentrates)
Kobe kwa kawaida hula majani na mboga mboga, uyoga, wadudu na minyoo. Pia unaweza kuwapa chakula cha mbwa (kidogo) kama chakula cha ziada.

KUKU-(gallus gallus)